Institute of Languages (INSTL)

Permanent URI for this collection

Browse

Recent Submissions

Now showing 1 - 20 of 37
  • ItemEmbargo
    Uchanganuzi Linganishi wa Wahusika wa Kike Katika Riwaya ya Usiku Utakapokwisha na Riwaya ya Nguu Za Jadi.
    (Kabale University, 2024) Ainebyoona, Olivia
    Utafiti huu umeshughulikia Uchanganuzi Linganishi wa Wahusika wa Kike Katika Riwaya ya Usiku Utakapokwisha na Nguu za Jadi. Tatizo la utafiti lilikuwa suala la kulinganisha matendo na lugha ambayo wahusika hawa wa kike katika kazi hizi halijashughulishwa. Lengo kuu lilikuwa kuchanganua wahusika wa kike katika riwaya teule. Sampuli ilikuwa riwaya ya Usiku Utakapokwisha ya Mbunda Msokile na riwaya ya Nguu za Jadi ya Clara Momanyi. Mtafiti ametumia mbinu ya uchambuzi matini na ushuhudiaji katika kukusanya data za utafiti. Matokeo yote kama wahusika wa kike kama vile Mangwasha mhusika mkuu katika riwaya nzima, Mbungulu na Mbwashu katika riwaya ya Nguu za Jadi.Vile vile kuna mhusika Nelli, Koleta na Klotilda ambao ni muhimu kataika riwaya ya Usiku Utakapokwisha, utofautiano wa matendo ya wahusika ni kama uvivu, ufanya kazi, kushauri, kutukana na kuleta mabadiliko na ufanano wa lugha ni kama lugha nyororo na lugha yenye hisia. Mapendekezo ni kufanywa kwa tafiti nyingine ili kulinganishwa na utafiti huu pamoja na kufanya utafiti wa kwenda uwanjani.
  • ItemEmbargo
    Uchunguzi Linganishi wa Usawiri wa Mwanamke Katika Jamii ya Wanyankore na Tamthilia ya Mama Ee Ya Ari Katini Mwachofi.
    (Kabale University, 2024) Akampamya, Mauricia
    Utafiti huu ulihusu Uchunguzi linganishi wa usawiri wa mwanamke katika jamii ya Wanyankore na katika tamthilia ya Mama ee iliyoandikwa na Ari Katini Mwachofi. Kwa kutumia mbinu ya mahojiano, mtafiti alipata data za lengo la kwanza na la tatu. Kwa kutumia mbinu ya uchanganuzi nyaraka, mtafiti alipata data za lengo la pili na la tatu. Sampuli ya watu kumi na watano yaani wanawake watano kutoka kila kijiji teule katika kata la Ruhaama ndio walifanya kama watoa taarifa pia data nyingine zikatolewa kwa tamthilia ya Mama ee iliyoandikwa na Ari Katini Mwachofi. Matokeo ni kwamba Jamii ya Wanyakore mwanamke anadunishwa ingawa kwa upande mdogo anakweza, pili yalionyesha kwamba mwanamke katika Tamthilia ya Mama ee anatwezwa kwa upande mkubwa.Mtafiti anapendekeza kwamba tafiti nyingine zifanywe kuhusu suala hili kwa kuangazia tamthilia,riwaya,diwani na tungo nyingine za kifasihi ili kuwepo uelewekaji wake zaidi.
  • ItemEmbargo
    Changamoto Za Mtalaa Mpya Katika Ufundishaji Wa Lugha Ya Kiswahili Kwa Walimu Shule Za Upili, Wilayani Kasese.
    (Kabale University, 2024) Biira, Janet
    Utafiti huu ulitazamia kushughulikia changamoto za mtalaa mpya katika ujifunzaji na ufundishaji wa lugha Kiswahili kwa walimu wa shule za upili wilayani kasese. Malengo ya utafiti huu yalikuwa kuchunguza changamoto za mtalaa mpya katika ufundishaji wa lugha ya Kiswahili, kutambua mabadiliko yaliyopo kati ya mtalaa mpya na mtalaa wa zamani, kuchunguza mikakati mbalimbali inayoweza kuwekwa ilikufanikisha ufundishaji wa lugha ya Kiswahili katika mtalaa wa mpya. Maswali ya utafiti huu yalikuwa; kwanza, mtalaa mpya unachangamoto zipi katika ufundishaji na ujiunzaji wa lugha ya kiswahi? Pili, je, kuna mabadiliko yoyote kati ya mtalaa mpya na mtalaa wa zamani? Tatu, ni mikakati ipi inayoweza kuwekwa ili kufanikisha ufundishaji wa na ujifunzaji wa wa lugha ya Kiswahili katika mtalaa mpya? Utafiti huu ulitumia utaratibu wa ukusanyaji data nyanjani au uwanjani kwa kutumia mbinu ya mahojiano. Vile vile, hojaji ilitumiwa (wanafunzi wa lugha ya Kiswahili). Mtafiti alitumia jumla ya shule sita mkiwemo shule ya upili ya Bwera, shule ya upili ya Karambi, shule ya upili ya St. Charles, shule ya upili ya Nyabugando Baptist, shule ya upili ya Hillside na ile ya Alliance zipatikanzo katika wilaya ya Kasese. Pia, mtafiti alitumia jumla ya shule sita za upili ambapo tatu zilikuwa ni za serekali na nyingine mbili ambazo ni za kibinafsi katika ukusanyaji wa data ya utafiti wake. Isitoshe, kutokana na matokeo ya utafiti huu yalidhihirisha kuwa kuwa kuna changamoto mbalimbali zilizotokana na mtalaa mpya mkiwemo; ukosefu wa vifaa vya kufundishia kama vitabu, upungufu wa vipindi vya Kiswahili, wanafunzi kulazimishwa kufanya miradi katika somo la Kiswahili na ukosefu wa walimu katika baadhi ya sehemu nchini Uganda. Pia utafiti huu kupitia data zake za uwanjani zilidhihirisha mabadiliko yafuatayo katika mtalaa mpya; kupunguka kwa vipindi, masomo yote kuchukua mfumo wa umilisi, wanafunzi kuchukua sehemu kubwa katika ufundishaji na ujifunzaji na kufanya miradi. Kuhusu mikakati ya kuweza kufanikisha ufundishaji katika mtalaa mpya hno ni kuwaruhusu wanafunzi kutumia Kiswahili katika mawasiliano yao ya kila siku, kutumia vifaa halisi na walimu kama vya kiteknolojia, kufundisha sarufi vilivyo. Mwisho kabisa, utafiti huu umetoa mapendekezo mbalimbali kwa walimu na wizara ya elimu kama kuongeza vipindi kwnye ratiba angalau vine kila wiki na kila kidato, wizara ya elimu kutoa vifaa vya kutosha vya kufundishia, wazazi na wakuu washule kuarifia kuhusu umuhimu/nafasi ya Kiswahili katika jumuiya Afrika Mashaariki, walimu kuongoza wanafunzi katika vipindi vya Kiswahili ipasavyo. Haya yakizingatiwa, yanaweza kuleta mabadiliko katika ufundishaji wa Kiswahili katika mtalaa mpya wa shule za upili.
  • ItemEmbargo
    Mchango Wa Methali Za Kiswahili Katika Kukuza Umilisi Wa Lugha Ya Kiswahili Kwa Wanafunzi Wa Shule Za Upili Wilayani Ntungamo.
    (Kabale University, 2024) Katsigaire, Joshua
    Mada ya utafiti huu ilikuwa ni Mchango wa Methali za Kiswahili katika Kukuza Umilisi wa Lugha ya Kiswahili kwa Wanafunzi wa shule za Upili Wilayani Ntungamo. Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa ni kuchunguza mchango wa methali za Kiswahili katika kukuza umilisi wa lugha ya Kiswahili kwa wanafunzi wa shule za upili wilayani Ntungamo. Kwa kutumia njia ya Mahojiano mtafiti alipata data za lengo la kwanza na za lengo la pili,sampuli iliyotumiwa ni shule za upili nne (4) na wanafunzi arobaini (40) wa kidato cha tatu wanaosoma lugha ya Kiswahili, ili kupata lengo la kwanza na la pili,methali mbali mbali za Kiswahili zinanokuza umilisi wa lugha zilikusanywa halafu na kuchunguzwa ili kupata ujumbe uliyomo kwa hali ya kutimiza lengo la pili la kufafanua ujumbe uliyomo katika methali za Kiswahili zinzofundishwa kwa wanafunzi wa shule za upili wilayani Ntungamo. Matokeo ya utafiti yanaonyesha kwamba zipo methali nyingi za Kiswahili ambazo huchangia katika kukuza umilisi wa wamafunzi wa lugha ya Kiswahili na methali hizo wanafunzi wanazijua tuu kimuundo lakini kifasihi hawazielewi kwa mfano,Mwacha asili ni mtumwa,Aliye juu mngoje chini,na Kidole kimoja hakivunji chawa. Pia matokeo ya methali yanaonyesha kwamba katika shule za upili Maanisipa ya Ntungamo, walimu wa Kiswahili wanajaribu kuwafunza wanafunzi wa kidato cha pili methali za Kiswahili ili wapate ujumbe uliyomo kwa ajili ya kutimiza lengo la pili. Utatiti huu ulikuwa ni wa kiwango cha shahada ya awali, ulichunguza methali chache tu kutoka shule za upili wilayani Ntungamo. Methali zilizokusanywa zinaakasi umulisi wa lugha ya Kiswahili. Utafiti mwingine wa kina kiwango cha Umahiri unapendekezwa kufanywa ili kupata michango mbali mbali nyingine ya methali za Kiswahili zinazokuza umilisi wa lugha ya Kiswahili .Ni imani yetu kwamba, tulichokipata uwandani kinaweza kuwa ni fununu tu juu ya mambo mengi yalifichama katika methali za Kiswahili. Utafiti huu unapendekezwa kwa kiwango cha shahada ya umahiri, unaweza kufanywa ili kupata michango mbali mbali nyingine ya methali za Kiswahili zinazokuza umilisi wa Lugha ya Kiswahili.
  • ItemEmbargo
    Embaganisa Eziriho Ahagati Y’ebigambo By'orunyankore N'eby’orukiga.
    (Kabale University, 2024) Ayebazibwe, Stephen
    Ebi mpandiikire omu kucondooza oku nibyoreka embaganisa eziriho ahagati y’ebigambo by’Orunyankore n’Orukiga omu bagambi b’endimi ezi. Nyine obwesigye ngu ebi ncondoorize nibiza kuyamba abashomi b’ebitabo, abeegi, nangwa n’abantu ba butoosha kwetegyereza oku ebigambo by’Orunyankore birikutaana n’eby’Orukiga omu miringo etari emwe n’emwe eyorekirwe. Okucondooza oku kugyendereire kuhwera abagambi b’Orunyankore n’Orukiga, nangwa n’abagambi b’endimi ezindi, kumanya embaganisa eziriho ahagati y’ebigambo by’endimi ezi ibiri nobu zirikuhuriza munonga.
  • ItemEmbargo
    Usawiri Wa Mwanamke Katika Methali Za Kikonzo.
    (Kabale University, 2024) Ithungu, Roseline
    Utafiti huu ulihusuUsawiri wa mwanamke katika methali za Kikonjo.Utafiti huu ulifanyiwa katika kata la Bwera wilayani Kasese. Kwa kutumia njia ya mahojiano, sampuli ya wazee ishirini (20) wenye umri wa miaka hamsini hadi juu ilitumiwa ili kufikia lengo la kwanza la pili na la tatu. Methali mbali mbali za Kikonjo zilikusanywa na kutengenezewa tafsiri isiyo rasimi katika Kiswahili ili kutimiza lengo la kwanza.Ili kufikia lengo la pili, uchunguzi makinifu ulifanywa na mtafiti akishirikiana na wazee ili kuona jinsi mwanamke anavyosawiriwa katika methali hizo kwa mfano kama asiye na mapenzi ya dhati, chombo cha starehe, mtumwa, mvivu, na mtu asiye na siri na kadhalika. Kwa lengo la tatu, mtafiti alifanya mahojiano kwa wazee ili kupata sababu za mwanamke kusawiriwa anavyosawiriwa katika methali za Kikonjo kwa mfano utamaduni, diini, tabia za mwanamke, na kadhalika.
  • ItemEmbargo
    Uchambuzi Wa Maneno Ya Kiswahili Kwenye Vyombo Vya Usafiri Na Athari Zake Kwenye Maendeleo Ya Kiswahili Katika Wilaya Ya Kasese.
    (Kabale University, 2024) Masereka, Elias Biseso
    Utafiti ulihusu uchanganuzi wa maneno ya Kiswahili kwenye vyombo vya usafiri kuhusu ukuzaji wa Kiswahili katika wilaya ya Kasese. Utafiti huu uliongozwa na malengo kama vile kuchunguza mchakato wa maneno ya Kiswahili katika usafirishaji katika wilaya ya Kasese, kutathmini juhudi za maneno yanayohusiana na usafiri ndani ya Kiswahili katika wilaya ya Kasese, na kutathmini mapendekezo ya kukuza uunganishaji sawia wa msamiati unaohusiana na usafiri. katika Kiswahili wilayani Kasese. Utafiti ulitumia watu 40 kama saizi ya sampuli kutoka kwa watu 60 waliolengwa. Utafiti ulitumia muundo wa utafiti wa kimaelezo. Matokeo ya utafiti yanaonyesha kuwa katika usafiri wa umma, istilahi za Kiswahili zinaanza kuonekana sambamba na lugha za kienyeji au Kiingereza. Kwa mfano, neno "matatu” linaweza kupitishwa pamoja na neno la ndani kwa magari hayo.Utafiti ulihitimisha kuwa kuna haja ya kuunganishwa kwa msamiati wa Kiswahili kwenye vyombo vya usafiri huakisi utanzu wa lugha na uanuwai wa kitamaduni uliopo katika wilaya. Utangamano huu ni mfano halisi wa jinsi Kiswahili, kama lugha inayozungumzwa na watu wengi katika Afrika Mashariki, kinavyoendelea kupenyeza nyanja mbalimbali za maisha ya kila siku, ikiwa ni pamoja na usafiri. Hatimaye, uchanganuzi unasisitiza umuhimu wa kutambua na kutumia anuwai ya lugha iliyopo katika Wilaya ya Kasese kama kichocheo cha maendeleo ya kijamii na kiuchumi na uboreshaji wa kitamaduni. Utafiti unapendekeza kwamba kuna haja ya kuanzisha istilahi sanifu za Kiswahili kwa ajili ya msamiati unaohusiana na usafiri kwa kushirikiana na wataalamu wa lugha, viongozi wa jamii na wadau wa usafirishaji Kuandaa programu za elimu na mafunzo ili kuboresha ustadi wa watoa huduma za usafiri, waelimishaji na wanajamii. Kampeni za Uzinduzi wa Kiswahili za kukuza matumizi ya Kiswahili katika usafirishaji na kuongeza ufahamu kuhusu umuhimu wake katika kukuza ushirikishwaji na utambulisho wa kitamaduni.
  • ItemRestricted
    Ulinganishaji wa Maisha Katika Tamthilia ya Mizigo Na Ya Jamii Wilayani Mbarara.
    (Kabale University, 2024) Turinawe, James
    Tamthilia Wamitila, (2002) katika Uhakiki wa fasihi ameeleza kuwa, neno tamthiliya kwa upana wake linatumiwa kujumuisha maneno drama na play ya Kiingereza. Kwa hiyo, tamthiliya ni utungo unaoandikwa kwa mtindo wa mazungumzo. Ubora wa fasili hii imezingatia kipengele cha mazungumzo ambacho ni kipengele muhimu katika tamthiliya. Wilaya ya Mbarara Wilaya ya Mbarara iko katika eneo la Magharibi mwa Uganda. Ilipakana na mkoa wa Ntungamo upande wa kusini, Wilaya ya Kiruhura upande wa mashariki, Wilaya ya Isingiro upande wa kaskazini-mashariki, na Wilaya ya Buhweju upande wa magharibi. Dhana ya Jamii Jamii ni msamiati ambao katika maisha ya kila siku tunautumia kuashiria maana fulani; ama, kulingana na muktadha au kwa maana halisi ya kileksia. Kamusi ya Kiswahili sanifu ya (2004) inafafanua kiduchu maana ya neno “Jamii” kuwa ni mkusanyiko wa watu au vitu. Vilevile, Kamusi ya Kiingereza Oxford Advanced Learner's Dictionary (2010), inafafanua kuwa Jamii ni watu kwa pamoja, waishio pamoja kwenye ujima; ni ujima fulani wa watu wenye desturi, tabia na sheria za aina moja. Simiyu (2011) katika Kitovu cha fasihi Simulizi anasema kuwa Jamii ni kikundi cha watu wanaotumia lugha moja, wana utamaduni mmoja na wanapatikana katika eneo moja la mastakimu. Kwa hiyo,kwa maoni yetu, ni sawa kabisa kufasili Jamii kama mkusanyiko au kundi la watu waliokusanyika sehemu fulani kama kijiji, kata, tarafa, wilaya, mkoa, kanda na taifa. Watu hawa huishi kama wamoja, na wenye kufuata utaratibu au kanuni fulani za kimaisha walizojiwekea wao wenyewe. Mkusanyiko huo wa watu unakuwa na utamaduni wake, unaodhihirika katika mila na desturi na mielekeo fulani ya kimaisha.
  • ItemRestricted
    Uchambuzi Wa Maneno Ya Kiswahili Kwenye Vyombo Vya Usafiri Na Athari Zake Kwenye Maendeleo Ya Kiswahili Katika Wilaya Ya Kasese.
    (Kabale University, 2024) Masereka, Elias Biseso
    Utafiti ulihusu uchanganuzi wa maneno ya Kiswahili kwenye vyombo vya usafiri kuhusu ukuzaji wa Kiswahili katika wilaya ya Kasese. Utafiti huu uliongozwa na malengo kama vile kuchunguza mchakato wa maneno ya Kiswahili katika usafirishaji katika wilaya ya Kasese, kutathmini juhudi za maneno yanayohusiana na usafiri ndani ya Kiswahili katika wilaya ya Kasese, na kutathmini mapendekezo ya kukuza uunganishaji sawia wa msamiati unaohusiana na usafiri. katika Kiswahili wilayani Kasese. Utafiti ulitumia watu 40 kama saizi ya sampuli kutoka kwa watu 60 waliolengwa. Utafiti ulitumia muundo wa utafiti wa kimaelezo. Matokeo ya utafiti yanaonyesha kuwa katika usafiri wa umma, istilahi za Kiswahili zinaanza kuonekana sambamba na lugha za kienyeji au Kiingereza. Kwa mfano, neno "matatu” linaweza kupitishwa pamoja na neno la ndani kwa magari hayo.Utafiti ulihitimisha kuwa kuna haja ya kuunganishwa kwa msamiati wa Kiswahili kwenye vyombo vya usafiri huakisi utanzu wa lugha na uanuwai wa kitamaduni uliopo katika wilaya. Utangamano huu ni mfano halisi wa jinsi Kiswahili, kama lugha inayozungumzwa na watu wengi katika Afrika Mashariki, kinavyoendelea kupenyeza nyanja mbalimbali za maisha ya kila siku, ikiwa ni pamoja na usafiri. Hatimaye, uchanganuzi unasisitiza umuhimu wa kutambua na kutumia anuwai ya lugha iliyopo katika Wilaya ya Kasese kama kichocheo cha maendeleo ya kijamii na kiuchumi na uboreshaji wa kitamaduni. Utafiti unapendekeza kwamba kuna haja ya kuanzisha istilahi sanifu za Kiswahili kwa ajili ya msamiati unaohusiana na usafiri kwa kushirikiana na wataalamu wa lugha, viongozi wa jamii na wadau wa usafirishaji Kuandaa programu za elimu na mafunzo ili kuboresha ustadi wa watoa huduma za usafiri, waelimishaji na wanajamii. Kampeni za Uzinduzi wa Kiswahili za kukuza matumizi ya Kiswahili katika usafirishaji na kuongeza ufahamu kuhusu umuhimu wake katika kukuza ushirikishwaji na utambulisho wa kitamaduni.
  • ItemRestricted
    Mchango Wa Mbinu Za Kufundisha Sarufi Ya Kiswahili Kwa Ubora Wa Mazungumzo Na Utendaji Wa Wanafunzi Wa Shule Za Upili Za Umma, Tukilenga Kaunti Ndogo Ya Kambuga Wilayani Kanungu Nchini Uganda.
    (Kabale University, 2019) Natushemereirwe, John
    Kusudi la utafiti huu lilikuwa ni kuchunguza mchango wa mbinu zinazotumika kufunza Lugha ya Kiswahili na umilisi wa mazungumzo ya wanafunzi katika lugha ya Kiswahili. Utafiti huu pia ulichunguza nafasi ya vifaa katika kufanikisha ufundishaji wa sarufi. Isitoshe, utafiti huu ulibainisha mazoezi wanayopewa wanafunzi ili kuimarisha sarufi na mazungumzo.
  • ItemEmbargo
    Changamoto Zinazokumba Wa Nafunzi Wa Vyuo Vya Juuwila Yani Kabale Nchiniuganda.
    (Kabale University, 2019) Ayebare, Rabecca
    Suala la changamoto zinazowak:umba wanafunzi limewavutia wataalamu wengi. Hata hivyo, hak:una utafiti mwingi ambao umefanyiwa juu ya changamoto zinazowakumba wanafunzi wa vyuo nchini Uganda. K wa hivyo, utafiti huu ulifanya uchunguzi juu ya changamoto zinazowakumba wanafunzikatika vyuonchini Uganda. Utafiti huu ulifanywa katika eneo la Munispaa ya Kabale wilayani Kabale Kusini Magharibi Uganda. Chanagamoto zinazowak:umba wanafunzi katika vyuo zilichunguzwa kwa kuangalia jinsia, miaka pamoja kozi mbali mbali zinazoshughulikiwa na wanafunzi mbali mbali katika vyuo vilivyofanyiwa uchunguzi katika somo hili.Madhumuni ya uchunguzi huu yalikuwa Kutambua asili ya changamoto zinazokumba wanafunzi katika vyuo, Kuchunguza jinsia ya wanafunzi ambao wanakumbwa hasana changamoto hizo nchini Uganda pamoja na Kubainisha njia za kukabiliana na changamoto zinazowakumba wanafunzi katika vyuo vya juu nchini Uganda kwa kulenga wilaya ya Kabale. Utafiti huu umeundwa na sura tano yaani sura ya kwanza, pili, tatu, nne na tano. Sura ya Kwanza imeshughulikia Utangulizi, Tatizo la utafiti, Malengo ya Utafiti, maswali ya utafiti Upeo wa utafiti, Umuhimu wa Utafiti na Changamotoza Utafiti.Sura ya Pili imeshughulikia Mapitio ya Kitaalama na ya yaliyoandikwa kuhusu changamoto zinazowakumba wanafunzi katika vyuo nchini Uganda pamoja na ujifunzaji wa Lugha ya Kiswahili.Imeelezea yaliyoandikwa kuhusu changamto zinazowakumba wanafunzi katika vyuo vya juu, mifumo ya elimu, aina za teknolojia na dhima ya teknolojia. Sura ya Tatu imezungumzia Njia na Mbinu za Utafiti.Imezungumzia Utangulizi, Eneo la Utafiti, Sampuli ya Utafiti na Usampulishaji, Ukusanyaji wa Data, Uchambuzi wa Data na Vifaa vya Utafiti.Sura ya Nne imeeleza juu ya Uwasilishaji na Uchambuzi wa data na hatimaye, sura ya tano ni muhtasari, matokeo muhimu, na mapendekezo ya ufiti huu.
  • ItemRestricted
    Okushoboorora Amatembezo Agu Orikurabamu Kuhinga Oburo Kuruga Aha Kububanjurira Ekishaka Kuhika Aha Kuburya.
    (Kabale University, 2022) Amutuhaire, Elias
    Ebi mpandiikire omu kucondooza oku nibyoreka bimwe aha matembezo agu orikurabamu kuhinga oburo kuruga aha kububanjurira ekishaka kuhika aha kuburya omuri Nyansoro, Kicuzi, Ibanda. Kandi ninyesiga ngu kuhwera abashomi n'abeegi ba butoosha kwetegyeereza gye rurimi orurikukoreesibwa omu bicweka bitari bimwe eby'amatembezo ogu orikurabamu kuhinga oburo kwiha aha kububanjurira ekishaka kuhika aha kuburya. Okucondooza oku kugyendereire kuhwera abo abatarikumanya amatembezo agu orikurabamu waaba noohinga oburo, ebi oshemereire kukora: kykrb; okwombera, okugyesha n'ebindi. Ekindi, okucondooza oku kugyendereire kuhisya aha beegi b'amatendekyero g'ahaiguru n'aha bantu abandi amatembezo agu orikurabamu omu kuhinga oburo kuhika aha kuburya, agu barikumanya n'agu batarikumanya, agu baarahuriireho nari agu batakahuriragaho.
  • ItemRestricted
    Dhia Ya Methali Ktika Ukuza.Ji Wa Nidhamu Baina Ya W Anajamii Kijijini BungandaroWilayanirubanda Nchini Uganda.
    (Kabale University, 2021) Atwinlramasiko, Ivan
    Utafiti huu ulikuwa na lengo la kuchunguza dhima ya methali katika ukuzaji wa nidhamu baina ya wanajamii kijijini Bungandaro, wilayani Rubanda nchini Uganda. Dhima za methal i katika ukuzaji wa nidhamu zilichunguzwa katika utafiti huu. Aid ha utafiti huu umeziainisha methali katika makundi matatu makuu, yaani uainishaji huu hutegemea maana ya ndani pamoja na maana ya nje na walengwa wa methali husika. Vile vile, methali zimeainishwa kulingana na maudhui ya kirnsingi yanayowasilishwa ndani ya methali hiyo hiyo, pamoja na uainisho wa kimafunzo. Makundi hayo ni pamoja na: Methali za kukashifu tabia mbaya miongoni mwa wanajamii, Methali za kuhimiza heshima kwa wazima miongoni mwa wanajamii pamoja na Methali za kuleta amani miongoni mwa wanajamii. Basi, makundi haya yote hukuza na kutimiza swala la nidhamu baina ya wanajamii. Utafiti huu umeundwa na sura tano yaani sura ya kwanza, pili, tatu, nne na tano. Sura ya Kwanza imeshughulikia Utangulizi, Tatizo la utafiti, Malengo ya Utafiti, Upeo wa utafiti, Umuhimu wa Utafiti na Changamoto zilizoukabili utafiti huu. Sura ya Pili imeshughulikia Mapitio ya Kitaaluma na ya Kazi tangulizi ambapo imeelezea yaliyoandikwa kuhusu methali na jinsi zinavyoweza kukuza nidhamu baina ya wanajamii. Aidha, imeelezea yaliyoandikwa kuhusu makundi parnoja na uanisho wa methali katika hali au masuala tofauti tofauti. Kadhalika, sura ya pili imeelezea Pengo la Maarifa na Kiunzi cha utafiti wa awali pamoja na jinsi utafiti huu ulivyoziba kiunzi au pengo fiilo. Sura ya Tatu imezungumzia Njia na Mbinu za Utafiti. Imezungumzia Utangulizi, Eneo la Utafiti, Sampuli ya Utafiti na Usampulishaji, Ukusanyaji wa Data. Uchambuzi wa Data na Vifaa vya Utafiti.Sura ya Nne imeeleza juu ya Uwasilishaji na Uchambuzi wa data,ambapo imeelezea aina za teknolojia ambazo huwa na dhima katika ukuzaji wa nidhamu. Sura ya tano imeeleza juu ya Muhtasari wa Utafiti na Mapendekezo.
  • ItemEmbargo
    Uhakiki Wa Mtindo Wa Lug Ha Ka Tika Riwaya Ya Ndoto Ya Almasi Na Ken Walibora.
    (Kabale University, 2022) Nuwamanya, Levinari
    Matini yoyote ya fasihi huhitaji kusomwa na kueleweka iii ipate kuwa na maana. Hata hivyo, kueleweka kwa matini hujitokeza ikiwa msomaji ataelewa mtindo uliotumika. Japo huu ndio ukweli, tafiti nyingi zilizofanywa hazijaangazia mtindo kama kipengele kinachojisimamia na tena maarufu katika kufafanua maudhui.Vipengele vya kimtindo pia vina ushirikiano na uhusiano mkubwa katika kupitisha ujumbe uliokusudiwa katika kazi ya kisanaa. Fauka ya hayo, matumizi mwafaka ya vipengele mbalimbali vya kimtindo huifanya kazi ya fasihi kuwa na mnato, mvuto na uzuri wa kipekee. Hata hivyo, matumizi mabaya ya mtindo hupelekea kazi ya kifasihi kukosa usanii na hata uzuri wake, yaani huwa chapwa na huathiri namna ujumbe unavyomfikia msomaji. Msanii yeyote anapokata shauri kuchagua vipengele fulani vya kisanaa sharti viweze kuvutia hadhira, kuchokonoa na kuathiri hisia zao. Mtindo unakuwa ni kigezo cha kupimia kufaulu au kutofaulu kwa msanii katika usanii wake. Mtunzi wa riwaya huhitaji weledi wa hali ya juu iii kuweza kufikia upeo wa ubunifu wake. Mapitio tangulizi ya maandishi yameonyesha kuwa hakuna utafiti uliofany wa kwa kina katika kubainisha mtindo kwenye riwaya ya Ndoto ya Almasi.
  • ItemEmbargo
    L'effet De L'environment Sur L'enseignement Et L'apprentissage De La Langue Francaise Dans Le District De Lira.
    (Kabale University, 2021) Oyugi, Jackson
    L'Ouganda est l'un des pays qui forment la communaute d'Afrique de l'Est. Deux pays de la communaute d'Afrique de l'Est; Le Burundi et le Rwanda ont utilise le francais comme langue officielle et comme moyen d'enseignement, bien que le Rwanda ait plus tard change la langue d'enseignement en anglais. Meme la Republique democratique du Congo, qui partageait directement des frontieres avec l'Ouganda, utilise le francais comme langue officielle et langue d'enseignement. L'etude vise specifiquement a decouvrir l'impact de l'environnement sur l'enseignement-apprentissage du francais a Lira.
  • ItemEmbargo
    Okushoboorora Aha Burugo Bwa Gamwe Aha Maziina G'abantu Agarikuk Wata Aha Naku N'okubonabona Omuri Ankole Disiturukiti Ya Ntungamo.
    (Kabale University, 2022) Nuwasiima, Patience
    Ebi mpandiikire omu kucondooza oku nibyereka gamwe aha maziina g'abantu agarikukwata aha naku n'okubonabona omuri Ankole, okukira munonga omuri Ntungamo-Disiturikiti, hamwe n'amakuru gaago, kandi niinyesiga ngu nibiija kuhwera abeegi hamwe n'enkunzi z'okushoma ebihandiiko bya Runyankore/Rukiga okumanya amakuru g'amaziina gaabo kandi n'okubaha amaziina againe amakuru, agubakubaasa kurondamu ag'okubatiza abaana baabo.
  • ItemRestricted
    Okurunda Ana Ebigambo Ebigumire Ebi Abahandiki Ba Runyankore-Rukiga Bakoreise, Amakuru N'enkoresa Yaabyo.
    (Kabale University, 2023) Atwine, Brendah
    Ebi mpandiikire omu kucondooza oku nibyooreka Ebigambo ebigumire ebi abahandiiki ba Runyankore-Rukiga bakoreise amakuru n'enkoresa yaabyo. Kandi nimpamya ngu nikiija kuhwera abashomi namunonga enkunzi z'orurimi kwetegyeereza gye amakuru g'ebigambo bitari bimwe ebitarikurahuka kwetegyerezibwa.Okucondooza oku kugyendereire kumanya hamwe n'okushoboorora bigambo ebigumire,amakuru n'enkoresa yaabyo kwenda ngu bimanywe nikwo byeyongyere kujanjaara n'okukoresibwa obutoosha.
  • ItemRestricted
    Mtazamo Wa Walimu Wa Kiswahili Ka Tika Shule Za Upili Kuhusu UbadilishaJi Wa Mtaala Wa Elimu Wilay Ani Kabale Nchini Uganda.
    (Kabale University, 2023) Akakikunda, Brenda
    Utafiti huu unahusu mtazamo wa walimu wa Kiswahili kuhusu ubadilishaji wa mtaala wa elimu nchini Uganda tukilenga wilaya ya Kabale. Utafiti huu ulibainisha mitazamo mbalimbali ya walimu na wanaelimu wengine, Changamoto zinazoweza kuukabili mtaala mpya pia na masuluhisho ya Changamoto zinazoweza kuukabili mtaala mpya huku tukifuatilia Malengo ya Utafiti huu. Utafiti huu ulifanyiwa katika shule mbalimbali Wilayani Kabale na shule hizo ni Kabale secondary school.St. Marys'College Rushoroza, Kigezi High School na BrainStorm High. Wahojiwa kumi ndio waliolengwa katika Utafiti huu kutoka katika Kila shule lililohusishwa yaani walimu watano na wanafunzi watano. Utafiti huu ulitumia muundo wa kimaelzo kutambua changamoto zinazoweza kukabili ubadilishaji wa mtaala. Mbinu za mahojiano, usomaji na usaili kukusanya data. K.upitia kwa vifaa vya hojaji na usaili wa moja kwa moja pamoja na usomaji. Nilipata changamoto kadhaa katika utafiti huu yaani; wanafunzi walikuwa hawajui kuongea Kiswahili ambacho kiliathiri mawasiliano, idadi ya wanafunzi ilikuwa nyingi ambacho kilinitatiza katika uchaguzi wa watafitiwa. Utafiti huu ulidhamiria kuwafaidi walimu wa K.iswahili iii kuwa na mtazamo mwema juu ya mtaala mpya ambacho kitawabidi kufanya iwezekanavyo kuona kwamba wanakidhi mahitaji ya mtaala mpya kwa kufuatilia maagizo ya mtaala mpya.
  • ItemRestricted
    Amakuru G'emiguutuuro N'enkozesa Yaa Yo Omu Runyankore -Rukiga Omuri Rukiga Disiturikiti Omu Igombororo Rya Rwamucuucu.
    (Kabale University, 2023)
    Ebicondoorize birooreka "Amakuru g'emiguutuuro n'enkozesa yaayo omu Runyankore-Rukiga". Kandi ndeesiga ngu biraza kuhwera abeegyesa, abeegi n'enkuzi z'orurimi okwetegyereza gye Amakuru g'emiguutuuro n'enkozesa yaayo omu Runyankore -Rukiga.
  • ItemEmbargo
    Methali Kama Kielezo Cha Shughuli Katika Jamii Ya Wahororo/ Wakiga Wilayani Rukungiri Nchini Uganda.
    (Kabale University, 2021) Nahurira, Ronnet
    Utafiti huu unahusu methali kama kielezo cha shughuli katika jamii ya Wahororo/ Wakiga wilayani Rukungiri, nchini Uganda. Hivyo ni kwamba somo hili liliongozwa na lengo kuu ambalo lilikuwa ni kubainisha shughuli zinazoelezwa na methali za kihororo pamoja na zile za Kikiga wilayani Rukungiri.Somo hili pia lilifuata malengo mahususi ambayo yalikuwa ni pamoja na: Kwanza, utafiti huu ulichunguza shughuli zinazoweza kuelezwa na methali katika Wahororo Wakiga nchini Uganda. Pili, utafiti huu ulibainisha uhusiano kati ya methali na matawi mengine ya fasihi simulizi na jinsi yanavyoweza kutumiwa kama kielezo cha shughuli za jamii ya Wahoro/Wakiga, nchini Uganda. Tatu, utafiti huu ulibainisha changamoto zinazokumba methali kama kielezo cha shughuli katika Wahororo/Wakiga wilayani Rukungiri pamoja na njia za kukabiliana na changamoto zinazokumba methali kutumiwa kama vielezo vya shughuli za Wahororo/ Wakiga wilayani Rukungiri. Utafiti huu ulifanyiwa wilayani Rukungiri katika vijiji vya Eisherero, Nyabihinga, Omukarere pamoja na Nyakashaka. Wahojiwa wazazi walitumiwa katika utafiti huu wakati wa kutoa data, walisaidia katika kutoa data kuhusu shughuli zinazoelezwa na methali pamoja na mifano ya methali zinazoeleza shughuli hizo. Utafiti huu uligundua kuwa ingawa methali hukumbwa na changamoto tofauti tofauti, zinarejelewa sana kama kielezo cha shughuli za Wahororo/Wakiga.