Mtazamo wa Umma Katika Ulazimishaji wa Ufundishaji wa Lug Hay a Kiswahili Nchini Uganda Tukilenga Wila Yaya Kasese ka Tika Tarafa ya Bwera.

Loading...
Thumbnail Image

Date

2021

Journal Title

Journal ISSN

Volume Title

Publisher

Kabale University

Abstract

Utafiti huu ulishughulikia Mtazamo wa umma katika ulazimishaji wa ufundishaji wa lugha ya Kiswahili nchiniUganda tukilenga wilaya ya Kasese katika tarafa ya Bwera. Utafiti huu ulikuwa na lengo kuu ambalo lilikuwa ni kubainisha mtazamo wa umma katika ulazimishaji wa ufundishaji wa lugha ya Kiswahili nchiniUganda. Hata hivyo, utafiti huu ulikuwa na malengo mahdsusi ambayo yalik:uwa ni: Kuchunguza mitazamo ya wanaumma, kiumri pamoja na kijinsia juu ya ulazimishaji wa ufundishaji wa lugha ya Kiswahili nchini Uganda, kubainisha changamoto zinazoweza kukabili ulazimishaji wa ufundishaji wa lugha ya Kiswahili nchini Uganda, kubainisha njia zinazoweza kuzingatiwa ili kukabiliana na changamoto zinazoweza kukabili ulazimishaji na ufundishaji wa lugha ya Kiswahili nchini Uganda. Utafiti huu uliundwa kwa sura tano, sura ya kwanza, sura ya pili, sura ya tatu, sura ya nne pamoja na sura ya tano. Sura ya kwanza inahusu usuli wa utafiti, suala la utafiti, malengo yaliyoongoza utafiti huu, maswali yaliyoongoza utafiti, upeo wa utafiti, umuhimu wa utafiti, changamoto zilizokabili utafiti pamoja na fasili ya istilahi muhimu zilizotumiwa katika utafiti huu uliohusu mtazamo wa umrna katika ulazizimishaji wa ufundishaji wav lugha ya Kiswahili nchini Uganda tukilenga wilaya ya Kasese katika tarafa ya Bwera .. Sura ya pili iliundwa na maandishi ya wataalamu pamoja na watafiti wengine, maoni haya ni yale ambayo yanahusiana na mada ya utafiti huu.Hata hivyo, maoni hayo yalikuwa na mchango mkubwa katika utafiti huu, ila 'yalikuwa na pengo zilizozibwa katika utafiti huu jvetu uliohusu mtazamo wa umma katika ulazimishaji wa ufundishaji wa lugha ya Kiswahili nchiniUganda tukilenga wilaya ya Kasese katika tarafa ya Bwera. Sura ya tatu ilihusiana na mbinu pamoja na vifaa vilivyotumika katika ukusanyaji wa data, enoo la utafiti, muundo wa utafiti, utaratibu wa kukusanya data, jumuiya na uteuzi wa sampuli ya utafiti, uhakikishaji wa ubora pamoja na uwanja wa utafiti. Sura ya nne, ilihusiana na uchambuzi pamoja na uwasilishaji wa data, Sura ya tano inahusiana na muhutasari, hitimisho mapendekezo ya utafiti pamoja na mapendekezo ya uchanganuzi zaidi katika utafiti huu. Hata hivyo, utafiti huu umeundwa kwa muundo wa kimaelezo, data zimekusanywa, kuchanganuliwa pamoja na kuwasilishwa katika maelezo ya lugha. Keywords: Mtazamo, Umma Katika Ulazimishaji, Ufundishaji, Lug Hay, Kiswahili Nchini, Tukilenga Kasese,Uganda.

Description

Keywords

Mtazamo, Umma Katika Ulazimishaji, Ufundishaji, Lug Hay, Kiswahili, Nchini, Tukilenga Kasese, Uganda

Citation